Kwa hiyo utawaambia: Mukisha kunitolea sehemu bora kuliko zote, sehemu itakayobakia itakuwa yenu, kama vile inavyokuwa kwa mulimaji anatwaa kinachobakia kisha kutoa sadaka zake za mazao ya kwanza ya ngano na zabibu.
Hamutakuwa na kosa lolote mukikula vitu hivyo, ikiwa kama mumemutolea Yawe sehemu bora kuliko zote, nanyi hamutachafua vitu vitakatifu vya Waisraeli na kufa.
Mukae ndani ya nyumba ile, nanyi mukule na kunywa chochote watakachowapa, kwa maana mutumishi anastahili kupewa mushahara wake. Musihame nyumba kwa nyumba.