Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Kwa hiyo utawaambia: Mukisha kunitolea sehemu bora kuliko zote, sehemu itakayobakia itakuwa yenu, kama vile inavyokuwa kwa mulimaji anatwaa kinachobakia kisha kutoa sadaka zake za mazao ya kwanza ya ngano na zabibu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:30
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.


Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.


Kuhani anapotakaswa, kilali na paja la kondoo dume wa utakaso vitaletwa na kutakaswa mbele yangu kwa kufanya kitambulisho cha kunitolea, navyo vitakuwa vya Haruni na wana wake.


Munaponitolea sadaka ya nyama anayekuwa kipofu, au kilema, au mugonjwa, huo si uovu? Mutawala atapendezwa au kukutendea mema ukimupa zawadi ya nyama kama yule? –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Kutokana na matoleo yote mutakayopokea, mutamutolea Yawe sehemu inayokuwa bora kuliko zote na takatifu.


Nanyi mutakula kilichotolewa mukiwa pahali popote pamoja na jamaa zenu maana ni mushahara wenu kwa sababu ya kazi yenu katika hema la mukutano.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ