Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:21
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.


Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”


Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo katika inchi ya Misri. Kila mwanainchi anapaswa kutoa sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa mufalme. Udongo wa makuhani tu ndio haukununuliwa na kufanywa mali ya mufalme.


na mule ndani wakaweka matoleo, sehemu moja za kumi na vyote vilivyotakaswa kwa uaminifu. Wakamuweka Konania, Mulawi, kuwa musimamizi mukubwa muchungaji wa vitu hivyo, na ndugu yake, Simea kuwa musaidizi wake.


Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu,


Kwa kufuata vile ilivyoandikwa katika Sheria kila muzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wana wetu, katika nyumba zetu, atapelekwa katika nyumba ya Mungu wetu kwa makuhani wanaotumika mule, vilevile tutapeleka kila muzaliwa wa kwanza dume wa ngombe zetu, mbuzi zetu na kondoo zetu.


Kila unga wetu wa kwanza, matoleo yetu, matunda ya miti, divai na mafuta tutavileta kwa kuhani kwenye vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Tena tutaleta zaka zetu za mazao yetu kwa Walawi, maana ndio wanaoshugulika na kukusanya zaka zile katika vijiji vyetu.


Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,


Watu wote wa Israeli, tangu wakati wa Zerubabeli na Nehemia, walitoa matoleo ya kila siku kwa ajili ya waimbaji na walinzi wa milango. Zaidi ya yote, watu wa Israeli wakatoa matoleo kwa ajili ya Walawi, nao Walawi wakatenga sehemu kwa ajili ya wazao wa Haruni.


Kisha, watu wote wa Israeli, wakaanza tena kuleta zaka zao za unga, divai na mafuta kwenye gala.


alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.


Hivyo mutajua kwamba nimewapa amri hii kusudi agano langu na ukoo wa Lawi likuwe la kudumu.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Ni mimi niliyewachagua wandugu zenu Walawi kati ya Waisraeli kama vile toleo kwenu. Wao wametengwa kwa ajili yangu mimi Yawe, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano.


Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.


Kisha kutokana na lile fungu la waaskari waliokwenda kwa vita, tenga sehemu ya kumi kwa ajili ya Yawe: kitu kimoja kutoka kila vitu mia tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo au mbuzi,


Mwenye kufundishwa Habari Njema anapaswa kushirikiana mapato yake na yule anayemufundisha.


Watapata mafungu yao sawa ya kula, ingawa wako na mapato kutokana na kuuzisha mali za jamaa zao.


Wazao wa Lawi wanaopewa kazi ya ukuhani wanaamriwa na Sheria kukongoa fungu moja la kumi la mapato toka kwa wandugu zao Waisraeli, ijapokuwa wao vilevile ni wa uzao wa Abrahamu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ