Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Yawe akamwambia Haruni: Wewe hautakuwa na urizi wowote katika inchi yao, wala kuwa na fungu lako kati yao; mimi ni fungu lako na urizi wako kati ya Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Nikiangalia kwa kuume kwangu na kungojea, ninaona hakuna mutu wa kunisaidia; sina tena nafasi ya kukimbilia, hakuna mutu anayenijali.


Wewe, ee Yawe, ndiwe riziki yangu kubwa, majaliwa yangu yako katika mikono yako.


Hata nikikosa nguvu katika mwili na katika roho, wewe, ee Mungu, ni kikingio changu; na hitaji langu lote ni wewe kwa milele.


Yawe ndiye sehemu yangu, hivyo nitamuwekea tumaini langu.


Makuhani hawatakuwa na haki ya kurizi inchi; haki yao ni kunitumikia mimi. Hamutawapa urizi katika inchi ya Israeli, watakachokuwa nacho ni mimi tu.


Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.


Hesabu ya Walawi wanaume wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na tatu. Hawa hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu wao hawakupewa urizi wowote kati yao.


Ndiyo maana kabila la watu wa Lawi halina sehemu ya inchi ya urizi pamoja na wandugu zao. Walichopokea ni heshima ya kuwa makuhani wa Yawe, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyoahidi.)


Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.


“Musiwasahau Walawi wanaoishi kati yenu; wao hawana fungu wala urizi wao kati yenu.


Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.


Musa hakuwapa watu wa kabila la Lawi inchi yoyote. Lakini sadaka za kuteketezwa kwa moto walizomutolea Yawe, Mungu wa Israeli, hizo ndizo zilizokuwa fungu lao, kama vile Yawe alivyomwambia Musa.


Lakini kabila la Lawi, Musa hakulipa sehemu yao ya inchi, maana aliwaambia kwamba sehemu yao itakuwa kumutumikia Yawe, Mungu wa Israeli.


Musa alikuwa ameyapa yale makabila mawili na nusu sehemu yao upande wa mashariki wa Yordani, lakini Walawi hawakukuwa wamepewa sehemu yao pamoja nao.


Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ