Hesabu 18:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Yawe akamwambia Haruni: Wewe hautakuwa na urizi wowote katika inchi yao, wala kuwa na fungu lako kati yao; mimi ni fungu lako na urizi wako kati ya Waisraeli.
Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.
Hesabu ya Walawi wanaume wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na tatu. Hawa hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu wao hawakupewa urizi wowote kati yao.
Ndiyo maana kabila la watu wa Lawi halina sehemu ya inchi ya urizi pamoja na wandugu zao. Walichopokea ni heshima ya kuwa makuhani wa Yawe, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyoahidi.)
Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.
Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.
Musa hakuwapa watu wa kabila la Lawi inchi yoyote. Lakini sadaka za kuteketezwa kwa moto walizomutolea Yawe, Mungu wa Israeli, hizo ndizo zilizokuwa fungu lao, kama vile Yawe alivyomwambia Musa.
Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”
Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.