Zahabu yote waliyomutolea Yawe kwa ajili ya kujenga hema takatifu ilikuwa na uzito wa kilo mia nane makumi saba na saba na grama mia tatu kulingana na vipimo vya hema takatifu.
Kila bei itapimwa kwa kipimo cha uzito cha shekeli kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu: uzito wa gera makumi mbili ni sawa na uzito wa shekeli moja.
Kila muzaliwa wa kwanza ambaye Waisraeli watanitolea, akiwa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu, au wa nyama, atakuwa wako. Lakini unaweza kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu, na kila muzaliwa wa kwanza wa nyama anayekuwa muchafu.
Lakini wazaliwa wa kwanza wa ngombe, kondoo au mbuzi wasikombolewe; hao ni watakatifu. Damu yao utainyunyizia mazabahu na mafuta yao utayateketeza kuwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ni harufu nzuri inayonipendeza mimi Yawe.