Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wazaliwa hao wa kwanza watakombolewa wakiwa wenye umri wa mwezi mumoja kwa kulipiwa feza shekeli tano, kulingana na vipimo vya hema takatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:16
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mumoja atakayehesabiwa anapaswa kulipa nusu ya shekeli kulingana na vipimo vya hema la mukutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea.


Zahabu yote waliyomutolea Yawe kwa ajili ya kujenga hema takatifu ilikuwa na uzito wa kilo mia nane makumi saba na saba na grama mia tatu kulingana na vipimo vya hema takatifu.


Kwa kupima uzito: gera makumi mbili ni shekeli moja, shekeli makumi tano ni mina moja.


Kila bei itapimwa kwa kipimo cha uzito cha shekeli kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu: uzito wa gera makumi mbili ni sawa na uzito wa shekeli moja.


Kila muzaliwa wa kwanza ambaye Waisraeli watanitolea, akiwa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu, au wa nyama, atakuwa wako. Lakini unaweza kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu, na kila muzaliwa wa kwanza wa nyama anayekuwa muchafu.


Lakini wazaliwa wa kwanza wa ngombe, kondoo au mbuzi wasikombolewe; hao ni watakatifu. Damu yao utainyunyizia mazabahu na mafuta yao utayateketeza kuwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ni harufu nzuri inayonipendeza mimi Yawe.


Kwa ajili ya malipo ya wazaliwa wa kwanza wanaume wa watu wa Israeli mia mbili makumi saba na watatu, wanaozidi hesabu ya wanaume Walawi,


utapokea kwa kila mwanaume feza shekeli tano, kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu, ambayo ni sawa na gera makumi mbili,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ