Hesabu 18:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Mazao yote ya kwanza ya matunda mabichi ya mashamba yao ambayo wataniletea mimi, yatakuwa yako. Kila mutu asiyekuwa muchafu katika jamaa yako anaweza kula.
Mutu mumoja akatoka Bali-Salisa, akamuletea Elisha mikate makumi mbili iliyotengenezwa kwa shayiri ya malimbuko ya mavuno ya mwaka ule na masuke mabichi ya ngano katika gunia. Elisha akamwagiza Gehazi awape watu wakule.
Mara tu amri hii ilipotolewa, watu wa Israeli wakatoa kwa wingi, malimbuko ya ngano, divai, mafuta, asali na mazao mengine mbalimbali ya shamba, na vilevile sehemu moja ya kumi ya kila kitu.
Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.
Ndani ya kikapu cha kwanza kulikuwa tini nzuri sana, kama vile tini za mavuno ya kwanzakwanza. Lakini ndani ya kikapu cha pili kulikuwa tini mbaya sana, mbaya hata hazifai kukuliwa.
Sehemu ya kwanza ya malimbuko yenu na vya matoleo yenu ya kila aina vitakuwa kwa ajili ya makuhani. Tena mutawapa sehemu ya kwanza ya unga wenu, kusudi mulete baraka juu ya nyumba zenu.
Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.
Kila jamaa italeta mikate miwili ya sadaka ya kutoa kwa kitambulisho mbele yangu mimi Yawe. Kila mukate utatengenezwa kwa kilo mbili za unga laini uliotiwa chachu na huo mutanitolea mimi Yawe ukiwa ni matoleo ya malimbuko yenu.
Ole wangu! Mimi ninakuwa kama muvunaji kisha wakati wa mavuno; hakuna tini za kwanzakwanza ninazotamani. Ni kama wakati wa kuchuma zabibu: hakuna hata fungu moja la zabibu la kula!
utatwaa malimbuko ya mazao utakayovuna katika inchi Yawe, Mungu wenu, anayokupa, na kuyaweka katika kikapu mpaka pale pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, amechagua pawe makao yake.