Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 18:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mutavikula vitu hivyo kama vitu vitakatifu kabisa, na ni wanaume tu ndio watakaovikula; vitu hivyo ni vitakatifu kwenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 18:10
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.


Mutaikula katika Pahali Patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazao wako kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hivi ndivyo nilivyoamuriwa.


Kwa nini hamukumukula katika Pahali Patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mulikuwa mumepewa huyo kwa kuondoa kosa ya Waisraeli wote pamoja na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe?


Kisha atachinja yule mwana-kondoo katika Pahali Patakatifu, wanapochinjia nyama wa sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka hii kwa ajili ya kosa na vilevile sadaka kwa ajili ya zambi, ni mali ya kuhani. Ni sadaka takatifu kabisa.


Mutu huyo anaweza kula mukate wa Mungu wake, vitu vitakatifu na vile vitakatifu kabisa.


Sadaka yoyote ya ngano iliyotolewa na kuhani itateketezwa yote; haitakuliwa hata kidogo.


Umwambie Haruni na wana wake kwamba hii ndiyo sheria ya ibada kuelekea sadaka kwa ajili ya zambi, pahali ambapo nyama wa sadaka ya kuteketezwa anapochinjiwa ndipo atakapochinjiwa nyama wa sadaka kwa ajili ya zambi, mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka takatifu kabisa.


Wanaoruhusiwa kula sadaka hiyo ni wanaume wa ukoo wa makuhani peke yao; ni sadaka takatifu kabisa. Itakuliwa katika Pahali Patakatifu.


Vilevile, vitu vingine vyote Waisraeli watakavyonitolea kama vile sadaka za kutikiswa, vitakuwa vyako. Ninakupa wewe, wana wako na wabinti zako kuwa haki yenu milele. Mutu yeyote katika jamaa yako asiyekuwa muchafu anaweza kula vitu hivyo.


Kati ya vitu vitakatifu kabisa ambavyo haviteketezwi kwa moto, hivi vitakuwa vyenu: sadaka za vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka za kosa. Kila kitu watu watakachonitolea kama vile sadaka takatifu kitakuwa chako na wana wako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ