Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 17:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 17:5
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wakati mufalme Uzia alipokuwa na nguvu, moyo wake akajaa kiburi ambacho kilisababisha maangamizi yake. Akamwasi Yawe wake kwa kuingia ndani ya hekalu akikusudia kufukiza ubani juu ya mazabahu.


Hao walitafuta ukoo wao katika kitabu cha ukoo, lakini hawakuonekana humo. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kushika ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu.


Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.


Tena, kesho asubui mutaona utukufu wa Yawe maana ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie?”


Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Itakuja siku wazao wa Yakobo watatoa mizizi; watu wa Israeli watachanua na kuchipuka, na kuijaza dunia yote kwa matunda.


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Nyumba zako wataziteketeza kwa moto na kuwafanya wanawake wengi waone azabu yako. Utakoma kujitoa kwa mutu yeyote afanye uzinzi nawe.


Nitaukomesha uasherati na uzinzi wako ulioufanya tangu ulipokuwa kule Misri. Hautaziangalia sanamu zozote tena wala kuifikiria tena inchi ya Misri.


Yawe anasema: Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu; nitawapenda tena kwa moyo wangu wote, maana sitawakasirikia tena.


Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.


Watu wakaanza kunungunika mbele ya Yawe juu ya taabu zao. Yawe akasikia, na hasira yake ikawaka. Moto toka kwa Yawe ukawaka kati yao na kuchoma upande mumoja wa kambi.


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


Kisha akamwambia Kora na wafuasi wake: Kesho asubui, Yawe ataonyesha ni nani anayekuwa wake na ni nani anayekuwa mutakatifu, na yule atakayemuchagua, atamuwezesha kukaribia kwenye mazabahu.


Ujitenge na watu hawa, niwaangamize mara moja! Lakini wao wakajitupa uso mpaka chini.


Kesho yake, Waisraeli wote pamoja wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Mumewaua watu wa Yawe.


Musa na Haruni wakakwenda, wakasimama mbele ya hema la mukutano,


Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.


Ninyi mutawaambia: ‘Sanduku la Agano la Yawe lilipopitishwa katika muto Yordani, maji ya muto huo yalizuiliwa yasitiririke!’ Kwa hiyo mawe haya yatakuwa ukumbusho kwa Waisraeli milele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ