Lakini moto umetoka kwenye shina lake, ukayateketeza matawi na matunda yake. Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo, wala hayatakuwa fimbo za kifalme. Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.
Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.
Vimekuwa vitakatifu kwa sababu watu hawa walivileta kwenye mazabahu ya Yawe. Basi, utwae vyetezo vya watu hao waliouawa kwa sababu ya zambi zao, vifuliwe kuwa vyembamba kusudi vikuwe kifuniko cha mazabahu. Hili litakuwa onyo kwa Waisraeli wote.
Siku Musa alipomaliza kusimamisha hema takatifu, akalimiminia mafuta na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote. Akamiminia mazabahu mafuta na kuitakasa pamoja na vyombo vyake vyote.