Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Basi, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi, na ule ugonjwa mukali uliowapata Waisraeli ikakoma.
Alipofika, akawaambia watu: Tafazali muondoke kwenye hema za watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, musiangamizwe pamoja nao kwa sababu ya zambi zao zote.
Basi, Yawe akamwambia Haruni: Wewe na wana wako na ukoo wako mutabeba lazima ya kazi za hema takatifu; vilevile na makosa yanayoambatana na ukuhani wako wewe mwenyewe na wana wako.
na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.
Yawe akawaka hasira juu ya Waisraeli, akawafanya watangetange katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine; kizazi kizima kilichokuwa kimefanya maovu mbele yake kikakufa.