Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 16:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Munaona ni jambo dogo kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewachagua ninyi kati ya Waisraeli wote, kusudi muweze kumukaribia na kutumika katika hema la Yawe na kushugulika na kutumikia Waisraeli wote?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 16:9
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Lea akamwambia kwa ukali: “Unazani ni jambo dogo kuninyanganya mume wangu na sasa unataka kutwaa dudai za mwana wangu?” Rakeli akamujibu: “Ikiwa utanipa dudai za mwana wako, Yakobo atalala kwako leo.”


Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako. Zaidi ya hayo, Bwana wangu Yawe, umeahidi kuchunga jamaa yangu kwa miaka mingi inayokuja na kunijulisha hivyo, ee Bwana wangu Yawe.


Pamoja na hayo, akawapa Walawi waliowafundisha watu wa Israeli na ambao walitakaswa kwa ajili ya Yawe, maagizo haya: “Muweke Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli aliyojenga; hamuhitaji kulibebabeba tena juu ya mabega. Sasa mumutumikie Yawe, Mungu wenu, na watu wake Waisraeli.


Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,


Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Wamoja kati yenu wanakula malisho mazuri na vilevile kukanyagakanyaga yale yaliyobaki. Wanakunywa maji safi na yanayobaki wanayachafua kwa miguu yao!


Hao tu ndio watakaoingia katika hekalu langu, nao watakaribia kwenye mazabahu kwa kunitumikia.


Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli.


Ni jambo dogo kwamba umetutoa Misri, inchi inayotiririka maziwa na asali, kusudi ukuje kutuua humu katika jangwa? Tena, unajifanya mukubwa wetu!


Musa akaendelea kumwambia Kora: Musikilize, enyi Walawi!


Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.


Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.


Siku moja walipokuwa wakifanya ibada, wakiwa wamefunga kula chakula, Roho Mutakatifu akasema: “Muwasimike Barnaba na Saulo kwa kazi ile niliyowachagulia.”


Kwa ngambo yangu, si neno hata kidogo kuhukumiwa nanyi au na tribinali ya watu. Na hata mimi mwenyewe sijihukumu.


Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.


Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ