Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa, imepanua kinywa chake mpaka mwisho. Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema wanaingia humo makundi kwa makundi, vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.
Kila mumoja wenu atwae chetezo chake, na kutia ubani, kisha atakipeleka mbele ya Yawe; kwa jumla vitakuwa vyetezo mia mbili makumi tano; wewe vilevile na Haruni, kila mumoja atakuwa na chetezo chake.
Lakini Yawe akifanya jambo ambalo halijapata kutendeka, udongo ukifunguka na kuwameza watu hawa pamoja na kila kitu chao, na kwenda kuzimu wakiwa uzima, basi mutajua kwamba watu hawa wamemuzarau Yawe.
Baba yetu alikufia katika jangwa na bila mutoto yeyote mwanaume. Yeye hakukuwa kati ya wafuasi wa Kora waliokusanyika mbele ya Yawe, lakini alikufa kutokana na zambi yake mwenyewe. Hakukuwa na mutoto mwanaume.
na mambo aliyowatendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu, mwana wa Rubeni. Mukumbuke jinsi mbele ya watu wote wa Israeli udongo ulivyofunguka na kuwameza pamoja na jamaa zao, mahema yao, nyama na watumishi wao wote.