Hesabu 16:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
26 Alipofika, akawaambia watu: Tafazali muondoke kwenye hema za watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, musiangamizwe pamoja nao kwa sababu ya zambi zao zote.
Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”
Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.
Na katika nyumba au muji wowote watakapokataa kuwakaribisha na kukataa kusikiliza maneno yenu, mutakapotoka kule mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu.
Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.
Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.