Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 16:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Ni jambo dogo kwamba umetutoa Misri, inchi inayotiririka maziwa na asali, kusudi ukuje kutuua humu katika jangwa? Tena, unajifanya mukubwa wetu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 16:13
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


“Heri Yawe angelituua tulipokuwa katika inchi ya Misri ambako tulikaa, tukakula nyama na mikate hata tukashiba. Lakini ninyi mumetuleta huku katika jangwa kwa kuua jamii hii yote kwa njaa!”


Lakini wote walikuwa na kiu, wakamunungunikia Musa wakisema: “Kwa nini ulitutoa kule Misri utuue kwa kiu, sisi wote na watoto wetu na mifugo yetu?”


Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?” Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!”


Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.


Wamoja kati yenu wanakula malisho mazuri na vilevile kukanyagakanyaga yale yaliyobaki. Wanakunywa maji safi na yanayobaki wanayachafua kwa miguu yao!


lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?


Kati ya Waisraeli kulikuwa kundi fulani lililoandamana nao ambalo lilikuwa na hamu kubwa ya kula nyama. Waisraeli wenyewe wakalia, wakisema: Heri kama tungeweza kupata nyama ya kula!


Tunakumbuka, samaki tuliokula katika Misri bila malipo, maboga, matikiti, mboga, vitunguu na vitunguu sumu!


Wakamwambia Musa: Tuliifikia inchi uliyotutuma tuipeleleze; hiyo ni inchi inayotiririka maziwa na asali, na hili ni tunda lake.


Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


Kwa nini Yawe anatupeleka katika inchi hiyo? Tutauawa katika vita, na wake zetu na watoto wetu watakamatwa mateka! Si afazali turudi Misri?


Musa akatuma ujumbe kwa Datani na Abiramu wana wa Eliabu kusudi waitwe, lakini wao wakasema: Hatutakuja!


Lakini wanainchi wenzake walimuchukia. Kwa hiyo wakatuma wajumbe kumufuata nyuma waende kusema: ‘Hatutaki mutu huyu kuwa mufalme wetu.’


“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ