Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 mutu atamutoa kama vile sadaka pamoja na sadaka ya vyakula ya unga wa kilo tatu unaokuwa muzuri na litre mbili za mafuta,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 15:9
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Ornani akamwambia Daudi: “Utwae kiwanja hiki, bwana wangu mufalme, na ukitumie vile unavyopenda mwenyewe. Angalia, ninawatoa ngombe dume kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, na vifaa vya kupepetea kwa kuni, pamoja na ngano ikuwe sadaka ya unga. Vyote hivyo ninakupa.”


Tunajiwekea sheria juu yetu kwamba, kwa mwaka tutatoa sehemu moja ya tatu ya kikoroti kimoja cha feza kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu:


Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.


Wakati wa siku za sikukuu na siku zilizopangwa, sadaka za unga zitakuwa litre kumi na saba zikiandamana na kila ngombe dume au kondoo dume, na chochote ambacho anayeabudu anaweza kutoa kwa kila mwana-kondoo. Kwa kila sadaka ya unga atatoa litre tatu za mafuta.


Mwana-kondoo, unga na mafuta vinapaswa kutolewa kila siku asubui kwa Yawe milele.


Pamoja na kila kondoo dume, ataleta sadaka ya unga litre kumi na saba na nusu, lakini pamoja na kila mwana-kondoo ataleta sadaka yoyote anayoweza. Na kwa kila sadaka ya unga, ataleta litre tatu za mafuta.


Pamoja na kila ngombe dume na kila kondoo dume anayetolewa sadaka, kunapaswa kuwa litre kumi na saba na nusu za unga, na pamoja na kila mwana-kondoo, kunapaswa kuwa chochote ambacho mufalme anatoa. Tena kwa kila sadaka ya unga, kunapaswa kutolewa litre tatu za unga.


Sadaka za vyakula na za kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Yawe. Makuhani, watumishi wa Yawe, wanaomboleza.


Labda Yawe, Mungu wenu, atabadilisha nia na kuwapa baraka ya mazao, mutaweza kumutolea sadaka za chakula na kinywaji.


Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.


Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.


Basi, hii ndiyo sheria kuelekea sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi, sadaka kwa ajili ya kosa, kuelekea kutakaswa na kuelekea sadaka ya amani.


pamoja na sadaka ya kinywaji ya litre mbili za divai, na kufanya harufu nzuri ya sadaka ya kumupendeza Yawe.


Wakati mutakapomutolea Yawe mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au sadaka kwa kutimiza kiapo au kwa ajili ya sadaka za amani,


Mutatoa sadaka ya vyakula ya unga laini kilo tatu, uliochanganywa na mafuta kwa kila ngombe dume mumoja; mutatoa kilo mbili za unga; kwa kila kondoo dume,


Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni litre mbili za divai kwa kila ngombe dume; litre moja na nusu kwa kila kondoo dume, na litre moja kwa kila mwana-kondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka muzima.


Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya mwezi mupya na sadaka yake ya vyakula, na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji kama vile inavyoagizwa. Itakuwa harufu nzuri yenye kupendeza; ni sadaka kwa Yawe iliyoteketezwa kwa moto.


Alipomwachisha kunyonya alimupeleka pamoja na ngombe dume wa miaka mitatu, gunia la unga na karabia ya divai. Hana alimwingiza mutoto kwenye nyumba ya Yawe kule Shilo, naye mutoto alikuwa mudogo tu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ