Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 15:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Katika vizazi vyote vinavyokuja, masharti yaleyale mutakayofuata ninyi ndiyo mugeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi atakayofuata; mbele ya Yawe mutakuwa sawa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 15:15
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutafuata sheria moja kila mutu atakayekosa bila kukusudia, akuwe ni mwanainchi Mwisraeli au ni mugeni anayeishi pamoja nanyi.


Ikiwa kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi na anapenda kufanya sikukuu ya Pasaka, mutu huyo sharti afanye hivyo kulingana na masharti na maagizo yote ya Pasaka. Kila mutu atafuata masharti yaleyale, akiwa mugeni au mwenyeji.


Sheria zilezile zitaelekea Mwisraeli aliyezaliwa katika inchi na wageni watakaoishi kati yenu.”


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Tangu siku ile Daudi alifanya uamuzi ule kuwa sharti na agizo katika inchi ya Israeli mpaka hivi leo.


Wazao wa Haruni, makuhani, ndio watakaopiga baragumu hizo. Utaratibu huo utakuwa sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu vyote.


Sheria hii inaelekea mugeni na mwenyeji. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Yawe akamwambia Musa na Haruni: “Haya ndiyo maagizo juu ya Pasaka. Mugeni yeyote hatashiriki chakula cha Pasaka.


Mushike jambo hili ninyi na wazao wenu kama agizo la milele.


Vizazi hata vizazi mutakumbuka tukio hilo kwa sikukuu kubwa kwa heshima yangu mimi Yawe. Hilo litakuwa agizo la milele kwenu.”


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


Yawe akamwambia Haruni: Ninakupatia matoleo Waisraeli waliyonipa, vitu vyote vitakatifu walivyonipa: vitu vyote vilivyotakaswa na Waisraeli. Ninakupa vitu vyote wewe na wazao wako kuwa fungu lenu, na hiyo ni haki yenu milele.


Na kama kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi kwa muda au siku zote, akitaka kutoa sadaka yake kwa kuiteketeza kwa moto, harufu inayomupendeza Yawe, mutu huyo atafanya kama vile munavyofanya ninyi.


Haruni na wana wake watavaa makapitula hizo kila mara wanapoingia katika hema la mukutano, au wanapokaribia kwenye mazabahu, kufanya kazi za makuhani katika Pahali Patakatifu. Kwa njia hiyo hawataonyesha uchi wao na kuwa na hatari ya kuuawa. Hilo ni sharti la kufuatwa siku zote kwa Haruni na wazao wake.


Waisraeli wote pamoja na viongozi wao, wazee na waamuzi na wageni wote waliokuwa kati yao, wakasimama kila upande kuelekeana na Sanduku la Agano mbele ya makuhani Walawi waliokuwa wamelibeba Sanduku la Agano la Yawe. Nusu yao wakasimama mbele ya mulima Gerizimu na nusu nyingine wakasimama mbele ya mulima Ebali, kama vile Musa, mutumishi wa Yawe alivyoagiza pale mbele juu ya kubarikiwa kwa Waisraeli.


Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ