Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.
Wakati walipokuwa wakiwaua, mimi niliachwa peke yangu, nikaanguka uso mpaka chini, nikalia: Ee Bwana wangu Yawe, utaangamiza watu wote wa Israeli waliobaki, ukitimiza kasirani yako juu ya Yerusalema?
Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.
Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?
Hapo, Musa na Haruni wakaondoka kwenye mukutano wa watu, wakaenda kusimama kwenye mulango wa hema la mukutano, wakainama uso mpaka chini. Basi, utukufu wa Yawe ukawatokea,
Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”
Naye akamujibu: “Wala wenu wala wa waadui zenu! Lakini mimi ni jemadari wa jeshi la Yawe, na sasa nimefika.” Yoshua akainama chini kwa heshima, kisha akamwuliza: “Bwana wangu, unataka mimi mutumishi wako nifanye nini?”
wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:
Na wamalaika wote waliokuwa wakizunguka kile kiti cha kifalme, wazee na vile viumbe vine vya ajabu, wakainama uso mpaka chini mbele ya kiti cha kifalme, nao wakamwabudu Mungu,