Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 14:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 14:22
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa miaka makumi mbili hii yote nimeishi katika nyumba yako. Nilikutumikia miaka kumi na mine kwa ajili ya wabinti zako wawili, na miaka sita nikachunga nyama wako. Lakini wewe, ukabadilisha mushahara wangu mara kumi.


Hata hivyo yeye amenidanganya na kubadilisha mushahara wangu mara kumi. Lakini Mungu hakumuruhusu kunizuru.


Mara hizi zote kumi mumenitukana. Basi, hamusikii haya kunitendea vibaya?


Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.


Hivyo Mungu akainua mukono, akaapa kwamba atawaangamizia katika jangwa,


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Wakamwambia Musa: “Hakukuwa makaburi ya kutosha katika inchi ya Misri hata ukatuleta tukufie huku katika jangwa? Kwa nini umetufanya tutoke katika inchi ya Misri?


Basi, watu wote wakamunungunikia Musa wakisema: “Sasa tutakunywa nini?”


Basi, Waisraeli wote pamoja wakamunungunikia Musa na Haruni kule katika jangwa. Wakasema hivi:


Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”


Lakini wote walikuwa na kiu, wakamunungunikia Musa wakisema: “Kwa nini ulitutoa kule Misri utuue kwa kiu, sisi wote na watoto wetu na mifugo yetu?”


Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”


Watu walipoona kwamba Musa amechelewa kurudi kutoka juu ya mulima, wakakusanyika mbele ya Haruni na kumwambia: Basi! Ututengenezee miungu itakayotuongoza, maana hatujui jambo lililomupata yule Musa aliyetutoa katika inchi ya Misri.


Basi, wakawaambia Musa na Haruni: “Yawe aone jambo hili na kuwahukumu ninyi kwa sababu mumetufanya sisi kuwa chukizo kwa mufalme wa Misri na wakubwa wake. Ninyi mumewapa sababu ya kutuua.”


Ninyi mumeona mambo mengi, lakini hamuelewi kitu. Masikio yenu yako wazi, lakini hamusikii kitu!


Jambo lolote la hekima au la maarifa ambalo mufalme aliwauliza alijionea mwenyewe kwamba vijana wale wane walikuwa bora mara kumi kuliko waaguzi na wachawi wote katika utawala wake.


Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.


Watu wakaanza kunungunika mbele ya Yawe juu ya taabu zao. Yawe akasikia, na hasira yake ikawaka. Moto toka kwa Yawe ukawaka kati yao na kuchoma upande mumoja wa kambi.


Kati ya Waisraeli kulikuwa kundi fulani lililoandamana nao ambalo lilikuwa na hamu kubwa ya kula nyama. Waisraeli wenyewe wakalia, wakisema: Heri kama tungeweza kupata nyama ya kula!


Kisha Miriamu na Haruni wakaanza kumusema Musa vibaya kwa sababu ya mwanamuke Mukushi aliyekuwa amemwoa.


Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?


Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


Wote hawataiona, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune wa ukoo wa Kenizi na Yoshua mwana wa Nuni, maana wao wamenitii kwa ukamilifu.


Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi vilevile: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”


Lakini, wengi sana kati yao hawakumupendeza Mungu, kwa hiyo wakakufia katika jangwa.


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


“Mukumbuke na musisahau jinsi mulivyomukasirikisha Yawe, Mungu wenu, kule katika jangwa. Tangu siku ile mulipotoka katika inchi ya Misri mpaka siku mulipofika pahali hapa, ninyi mumekuwa mukimwasi Yawe.


Kule babu zenu walinipima na kunijaribia, ingawa walikuwa wameona yote niliyotenda kwa muda wa miaka makumi ine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ