Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’
“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.