Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi, kwa agizo la Yawe, Musa akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya watu wa Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 13:3
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

nao Waisraeli wakaanza safari yao kutoka jangwa la Sinai. Wingu hilo likapanda na kisha likatua katika jangwa la Parani.


Nyuma ya hayo, watu wakafanya safari kutoka Haseroti, wakapiga kambi katika jangwa la Parani.


Tuma watu waende wapeleleze inchi ya Kanana ambayo ninawapa watu wa Israeli. Utatuma mutu mumoja kutoka katika kila kabila, na mutu huyo anapaswa kuwa kiongozi katika kabila lake.


Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.


Haya ndiyo majina ya watu hao kulingana na makabila yao: Kabila la Rubeni: Samua mwana wa Zakuri. Kabila la Simeoni: Safati mwana wa Hori. Kabila la Yuda: Kalebu mwana wa Yefune. Kabila la Isakari: Igali mwana wa Yosefu. Kabila la Efuraimu: Hosea mwana wa Nuni. Kabila la Benjamina: Palti mwana wa Rafu. Kabila la Zebuluni: Gadieli mwana wa Sodi. Kabila la Yosefu (ni kusema kabila la Manase): Gadi mwana wa Susi. Kabila la Dani: Amieli mwana wa Gemali. Kabila la Aseri: Seturi mwana wa Mikaeli. Kabila la Nafutali: Nabi mwana wa Wofusi. Kabila la Gadi: Geueli mwana wa Maki.


Hivi ndivyo walivyofanya babu zenu nilipowatuma kutoka Kadesi-Barnea kwa kupeleleza inchi.


Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni ndio watakaowagawanyia watu inchi kuwa mali yao.


“Basi, kama vile Yawe, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukaanza safari yetu kutoka mulima Horebu, tukapita katika lile jangwa kubwa la kutisha munalojua, kwa kufuata njia inayoelekea inchi ya milima ya Waamori. Tulipofika Kadesi-Barnea,


Jambo hilo likaonekana kuwa zuri kwangu, nikawachagua watu kumi na wawili, mutu mumoja kutoka katika kila kabila.


Na Yawe alipowatuma kutoka Kadesi-Barnea, akisema ‘Muende murizi inchi ambayo nimewapatia’, hamukufuata amri ya Yawe, Mungu wenu. Hamukuamini wala hamukutii yale aliyowaambia.


Sasa, Samweli akakufa. Nao Waisraeli wote wakakusanyika kwa kumwomboleza. Wakamuzika kwenye nyumba yake kule Rama. Kisha Daudi akaenda zake kwenye jangwa za Parani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ