Hesabu 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
26 Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.
“Basi, kama vile Yawe, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukaanza safari yetu kutoka mulima Horebu, tukapita katika lile jangwa kubwa la kutisha munalojua, kwa kufuata njia inayoelekea inchi ya milima ya Waamori. Tulipofika Kadesi-Barnea,
Siku moja watu wa kabila la Yuda wakamwendea Yoshua kule Gilgali. Kalebu mwana wa Yefune, ambaye alikuwa Mukenizi, akamwambia Yoshua: “Bila shaka unakumbuka jinsi Yawe alivyomwambia Musa, mutu wa Mungu, juu yangu na wewe tulipokuwa Kadesi-Barnea.
Nilipokuwa na umri wa miaka makumi ine, Musa mutumishi wa Mungu, akanituma kutoka Kadesi-Barnea, kwenda kuipeleleza inchi. Niliporudi nikamuletea habari za mambo ya kule kadiri nilivyoamini katika moyo wangu.