24 Pahali pale pakaitwa Bonde la Eskoli, ni kusema “Bonde la Shada” kwa sababu ya shada ambalo watu hao wa Israeli walikata kutoka pahali pale.
Walipofika katika Bonde la Eskoli, watu hao wakakata shada la muzabibu lililokuwa na matunda mengi nalo lilibebwa na watu wawili juu ya muti. Wakatwaa vilevile makomamanga na tini.
Kisha kupeleleza inchi kwa muda wa siku makumi ine, watu hao wakarudi.
Wao walikwenda mpaka bonde la Eskoli, wakaiona inchi, lakini waliporudi, wakavunja Waisraeli moyo kusudi wasiingie katika inchi Yawe aliyowapa.