Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Tuma watu waende wapeleleze inchi ya Kanana ambayo ninawapa watu wa Israeli. Utatuma mutu mumoja kutoka katika kila kabila, na mutu huyo anapaswa kuwa kiongozi katika kabila lake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 13:2
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.


Kiongozi mumoja wa jamaa kutoka kila kabila atakusaidia kufanya hesabu.


Basi, Yawe akamwambia Musa: Uwakusanye wazee makumi saba wa Israeli, ambao wewe unajua wanaheshimiwa na kukubaliwa na watu kuwa viongozi, uwalete kwenye hema la mukutano, wasimame karibu nawe.


Haya ndiyo majina ya watu ambao Musa aliwatuma kwenda kupeleleza inchi ya Kanana. Musa akamupa Hosea mwana wa Nuni jina jipya, akamwita Yoshua.


Basi, kwa agizo la Yawe, Musa akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya watu wa Israeli.


Hivi ndivyo walivyofanya babu zenu nilipowatuma kutoka Kadesi-Barnea kwa kupeleleza inchi.


Utatwaa vilevile kiongozi mumoja kutoka kila kabila kwa kusaidia katika ugawanyaji wa inchi.


Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.


Na Yawe alipowatuma kutoka Kadesi-Barnea, akisema ‘Muende murizi inchi ambayo nimewapatia’, hamukufuata amri ya Yawe, Mungu wenu. Hamukuamini wala hamukutii yale aliyowaambia.


Sasa, muchague watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, kila kabila mutu mumoja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ