na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Nitawapa malisho mazuri kwenye milima mirefu ya inchi ya Israeli ambako kuna mashamba mazuri ya kuwakulishia. Watapumzika huko kwenye mbuga za malisho mazuri; watapata malisho mazuri juu ya milima ya inchi ya Israeli.