Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.
Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.
Kesho yake, wakaamuka asubui mapema wakaenda sehemu za milima, wakisema: Sasa tuko tayari kabisa kwenda pahali ambapo Yawe alituahidi. Tunaitika kwamba tulitenda zambi.
Hapo, Waamori waliokuwa wanaishi katika eneo hilo la milima wakateremuka kuwashambulia na kama vile nyuki wanavyofanya wakawapiga huko Seiri mpaka Horma.
Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.
ukaendelea kwa kusini mpaka kwenye mwinuko wa Akarabimu, ukapitia pembeni ya Sini, na kusini ya Kadesi-Barnea, ukipitia Hesironi hata Adari na kisha ukageuka kuelekea Karaka.
Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.
Akamujibu: “Unipe zawadi! Ninaomba unipe chemichemi za maji maana kule upande wa kusini ni jangwa.” Kalebu akamupa chemichemi za upande wa juu na za chini.
Yawe alikuwa pamoja na watu wa kabila la Yuda, nao wakaiteka inchi ya milima. Lakini hawakuweza kuwashinda wenyeji wa inchi ya bonde kwa sababu magari yao ya vita yalikuwa ya chuma.