Musa akamwambia Yoshua: “Chagua wanaume uende upigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilele cha kilima, nikishika katika mukono wangu ile fimbo ya Mungu.”
Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.
Tuma watu waende wapeleleze inchi ya Kanana ambayo ninawapa watu wa Israeli. Utatuma mutu mumoja kutoka katika kila kabila, na mutu huyo anapaswa kuwa kiongozi katika kabila lake.
Kisha ile hema ikaachwa kwa kizazi cha babu zetu kilichofuata. Nao wakaibeba chini ya uongozi wa Yoshua mpaka waliponyanganya inchi ya mataifa yale Mungu aliyofukuza mbele ya kufika kwao. Nayo ikabaki katika inchi mpaka katika siku za Daudi.
Ni vile anavyosema katika maandiko haya ya nabii Hosea: “Wale waliokuwa si watu wangu nitawaita sasa ‘Watu wangu.’ Taifa lile nililokosa kulipenda nitaliita sasa ‘Mupendwa wangu.’