Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 12:6
50 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.


Kisha Yakobo akaamuka toka usingizi, akasema: “Hakika, Yawe yuko pahali hapa, nami sikujua!”


Usiku mumoja, Yosefu akaota ndoto, lakini alipowaelezea wandugu zake, wao wakazidi kumuchukia.


Kisha Yosefu akaota ndoto ingine, akawaelezea wandugu zake akisema: “Musikilize, nimeota ndoto nyingine. Nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinainamia mbele yangu.”


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Lakini usiku uleule neno la Yawe lilimufikia Natani kusema hivi:


Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.


Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


Mungu anaongea na watu katika ndoto na maono, wakati usingizi muzito unapowapata,


Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto, wakati usingizi muzito unawashika watu.


“Musiwaguse wachaguliwa wangu; musiwazuru manabii wangu!”


Ee Yawe, ngao yetu ni chini ya ulinzi wako. Mufalme wetu ametoka kwako, ewe Mutakatifu wa Israeli.


Yawe akamwambia Musa: “Mimi ninakufanya kuwa kama mungu kwa mufalme wa Misri, naye ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako.


Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!


Nabii aliyeota ndoto, atangaze ndoto yake, lakini yule aliyefunuliwa ujumbe wangu autangaze kwa uaminifu. Kuna ulinganifu gani kati ya maganda na ngano? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Hivyo, niliachwa peke yangu nikiangalia hayo maono ya kushangaza. Nguvu zikaniishia, na uso wangu ukabadilika rangi, nikabaki bila nguvu.


Halafu Danieli akafunuliwa fumbo hilo usiku katika maono. Naye Danieli akamushukuru Mungu wa mbinguni,


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:


Katika maono haya, nilijikuta niko Susani, muji mukubwa wa jimbo la Elamu. Nilikuwa nimesimama kando ya muto Ulayi.


Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.


Kisha mambo hayo nitashusha Roho wangu juu ya watu wote. Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu, mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Herode alipokuwa amekwisha kufa, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto kule Misri.


Hivi munajishuhudia ninyi wenyewe kuwa ninyi ni ukoo wa watu waliowaua manabii.


Kwa sababu hiyo, nitawatumia manabii na watu wenye hekima na walimu. Mutawaua wamoja wao, mutatundika wengine juu ya misalaba, mutawapiga wengine fimbo ndani ya nyumba zenu za kuabudia na kuwafukuza muji kwa muji.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”


Halafu malaika wa Bwana akamutokea Zakaria, akisimama upande wa kuume wa mazabahu ya kuchomea ubani.


Alipotoka inje, hakuweza kusema nao, na watu wakatambua kwamba amepata maono ndani ya hekalu. Lakini alikuwa akifanya alama kwa mikono, kwa sababu alibaki bubu.


Lakini vilevile hatuwezi kusema kwamba yalitoka kwa watu, kwa maana watu wote watatutupia mawe, kwa sababu wanasadiki kwamba Yoane alikuwa nabii.”


Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine.


Petro alipokuwa angali na wasiwasi, naye akijiuliza juu ya maana ya maono yale, wale watu waliotumwa na Kornelio wakafika mbele ya mulango kwa maana walikuwa wamekwisha kujulishwa nafasi gani kunapokuwa nyumba ya Simoni.


Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Hata alipomwomba Yawe shauri, Yawe hakumujibu kwa ndoto, kwa mawe ya kupiga kura, wala kwa njia ya manabii.


Samweli akalala pale mpaka asubui, kisha akaamuka na kufungua milango ya nyumba ya Yawe. Lakini Samweli aliogopa kumwambia Eli maono hayo.


Yawe alizidi kujionyesha kule Shilo, ambako alimutokea Samweli na kuongea naye. Naye Samweli aliposema kitu, Waisraeli wote walimusikiliza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ