Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wakasema: Basi, Yawe amezungumuza kwa kumwagiza Musa peke yake? Si amezungumuza nasi vilevile? Yawe akasikia maneno hayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 12:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lea akapata mimba tena, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Simeoni, akisema: “Yawe amenipa mutoto mwingine mwanaume kwa sababu amesikia jinsi ninavyochukiwa.”


Muda wa kufunga kilio ulipokwisha, Daudi aliagiza wamulete Batiseba na kumupeleka katika nyumba yake. Batiseba akakuwa muke wa Daudi, naye akamuzalia Daudi mutoto mwanaume. Lakini jambo hilo Daudi alilofanya lilimuchukiza Yawe.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


Halafu hasira ya Mungu ikawaka juu ya Musa, akamwambia: “Si kuna ndugu yako Haruni ambaye ni Mulawi? Ninajua yeye anajua kusema vizuri. Tena anakuja kukutana nawe, na mara tu atakapokuona atafurahi ndani ya moyo.


Haruni akawaambia maneno yote Yawe aliyokuwa amemwagiza Musa na kufanya vile vitambulisho mbele ya watu wote.


Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kufanya kama vile walivyoamuriwa na Yawe. Haruni akatupa fimbo yake chini mbele ya mufalme na wakubwa wake, nayo ikakuwa nyoka.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.


Watu wakaanza kunungunika mbele ya Yawe juu ya taabu zao. Yawe akasikia, na hasira yake ikawaka. Moto toka kwa Yawe ukawaka kati yao na kuchoma upande mumoja wa kambi.


Lakini Musa akamujibu: Unaona wivu kwa ajili yangu? Heri Yawe angewapa watu wake wote roho yake nao wapate kuwa manabii!


(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)


Wakakusanyika mbele ya Musa na Haruni, wakawaambia: Ninyi mumepitisha kipimo! Waisraeli wote pamoja ni watakatifu; kila mumoja ni mutakatifu. Yawe yuko pamoja nasi wote. Mbona sasa ninyi munajifanya wakubwa kushinda watu wengine wa Yawe?


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,


Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ