Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Hapo, Yawe akashuka katika wingu na kuzungumuza naye. Halafu akatwaa sehemu ya roho aliyokuwa amemupa Musa, akawapa kila mumoja wa wale wazee makumi saba. Walipoingiwa na roho huyo, wazee hao wakaanza kutoa unabii, lakini hawakurudia kufanya hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:25
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.


Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria; ukawapa mana kuwa chakula chao, na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.


Alisema nao katika nguzo ya wingu; walitimiza maagizo yake na masharti aliyowapa.


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


Yawe akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Musa, akataja jina lake: Yawe.


Katika safari zao zote, Waisraeli waliweza kuliona lile wingu la Yawe juu ya hema wakati wa muchana na ule moto ukiwaka juu yake usiku.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Na mbele yao kulikuwa wazee makumi saba wa taifa la Waisraeli pamoja na Yazania mwana wa Safanu. Kila mumoja alikuwa na chetezo katika mukono, na moshi wa ubani ulipanda juu.


Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.


Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele.


Basi, Musa akaenda kwa Datani na Abiramu, akifuatwa na wazee wa Israeli.


akainua macho, akawaona Waisraeli wamepiga kambi kila kabila pahali pake. Kisha Roho ya Mungu ikamufikia,


Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake,


Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)


Zawadi ya unabii inapaswa kuwa chini ya utawala wa yule aliyeipewa,


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Maana hakuna hata ujumbe wowote uliotetewa kwa mapenzi ya kimutu, lakini watu walipasha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mutakatifu.


Basi, roho wa Yawe akamujaza Otinieli, naye akakuwa mwamuzi wa Waisraeli. Otinieli alikwenda katika vita naye Yawe akamutia Kusani, Yule-Mwovu-Sana, ufalme wa Mesopotamia, katika mikono yake.


Saulo na mutumishi wake walipofika kule Gibea, alipokelewa na kundi la manabii. Roho wa Mungu alimufikia kwa nguvu, na Saulo akaanza kutabiri pamoja na manabii hao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ