Hesabu 11:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
24 Basi, Musa akaenda na kuwajulisha watu yale Yawe aliyosema. Kisha, akakusanya wazee makumi saba kutoka kati ya wazee viongozi nao akawaweka kandokando kuzunguka hema.
Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.
Basi, Yawe akamwambia Musa: Uwakusanye wazee makumi saba wa Israeli, ambao wewe unajua wanaheshimiwa na kukubaliwa na watu kuwa viongozi, uwalete kwenye hema la mukutano, wasimame karibu nawe.
Wazee wawili kati ya wale makumi saba waliochaguliwa, Eldadi na Medadi, walikuwa wamebaki katika kambi wenzao walipokwenda kwenye hema. Roho iliwafikia humohumo ndani ya kambi, wakaanza kutoa unabii pahali walipokuwa.