22 Kunaweza kuchinjwa kondoo na ngombe wa kuwatosheleza? Samaki wote bahari wavuliwe kwa ajili yao?
Jemedari mulinzi wa mufalme akamwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Elisha akamujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”
Nitapata wapi nyama ya kuwakulisha watu hawa wote? Maana wanalia mbele yangu wakisema: Utupatie nyama tukule!
Lakini Musa akamwambia Yawe: Hesabu ya watu ninaowaongoza hapa ni elfu mia sita wanaoenda kwa miguu, nawe unasema: Nitawapa nyama ya kuwatosha mwezi muzima!
Yawe akamujibu Musa: Uwezo wangu umepunguka? Utaona basi kama neno langu litakuwa la kweli kwako au hapana.
Nao wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori, tutaweza kupata wapi chakula cha kushibisha kundi kubwa kama hili?”
Yesu akawajibu: “Ninyi wenyewe muwape chakula.” Lakini wakamwuliza: “Unataka tuende kununua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza?”
Wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori mutu ataweza kupata wapi chakula cha kuwashibisha?”
Zakaria akamwuliza yule malaika: “Kitu gani kitakachonijulisha kwamba maneno hayo ni ya kweli? Mimi ni muzee, na muke wangu amekwisha kuzeeka sana.”
Maria akamwuliza malaika: “Jambo hili litawezekana namna gani kwa maana mimi ningali bikira?”
“Hapa kuna mutoto mumoja anayekuwa na mikate mitano ya shayiri pamoja na samaki mbili. Lakini chakula hiki hakitawafalia kitu watu wengi kama hawa.”