Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:20
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo basi, kwa sababu umenizarau na umemutwaa muke wa Uria wa Hiti kuwa muke wako, mauaji hayataondoka katika jamaa yako.’


Naye akawapa kile walichoomba, lakini akaleta magonjwa makali kati yao.


Basi, kwa wakati wa magaribi kukakuja kwale wengi, wakafunika kambi ya Waisraeli. Asubui yake kukatokea umande, ukatanda kandokando ya kambi yao.


“Heri Yawe angelituua tulipokuwa katika inchi ya Misri ambako tulikaa, tukakula nyama na mikate hata tukashiba. Lakini ninyi mumetuleta huku katika jangwa kwa kuua jamii hii yote kwa njaa!”


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Aliyeshiba anakataa hata asali, lakini kwa mwenye njaa kila chakula kichungu ni kitamu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Nitapata wapi nyama ya kuwakulisha watu hawa wote? Maana wanalia mbele yangu wakisema: Utupatie nyama tukule!


Mutakula nyama si kwa muda wa siku moja tu, au mbili, au tano, au kumi au makumi mbili,


Lakini Musa akamwambia Yawe: Hesabu ya watu ninaowaongoza hapa ni elfu mia sita wanaoenda kwa miguu, nawe unasema: Nitawapa nyama ya kuwatosha mwezi muzima!


Kwa nini Yawe anatupeleka katika inchi hiyo? Tutauawa katika vita, na wake zetu na watoto wetu watakamatwa mateka! Si afazali turudi Misri?


Basi wakaanza kuambiana: Tuchague kiongozi, turudi Misri.


Ni jambo dogo kwamba umetutoa Misri, inchi inayotiririka maziwa na asali, kusudi ukuje kutuua humu katika jangwa? Tena, unajifanya mukubwa wetu!


Kwa nini mulituleta sisi watu wa Yawe huku katika jangwa? Mulituleta kusudi tukufe pamoja na mifugo yetu?


Basi, wakaanza kumunungunikia Mungu na Musa, wakisema: Kwa nini mumetutoa Misri tukuje tukufie humu katika jangwa? Humu hamuna chakula wala maji; nasi tumechokeshwa na chakula hiki cha bure.


‘Muangalie, ninyi wenye kuzarau, mupigwe na mushangao na mutoweke! Maana katika siku hizi nitafanya jambo ambalo ninyi musingeweza kusadikia hata wangewaelezea.’ ”


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Halafu akawaambia watu wote: “Jiwe hili ndilo litakalokuwa ushuhuda kwetu, maana limesikia maneno yote ambayo Yawe ametuambia. Kwa hiyo, litashuhudia juu yenu, kusudi musipate kumwasi Mungu wenu.”


Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ