Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Watu wakamulilia Musa, naye akamwomba Yawe na moto huo ukazimika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:2
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu alisema atawaangamiza watu wake, lakini Musa, muchaguliwa wake, aliingilia kati, akazuia hasira yake isiwaangamize.


Basi, Musa akaondoka kwa mufalme, akaenda kumwomba Yawe.


Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Mufalme Zedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Selemia, pamoja na kuhani Zefania mwana wa Maseya, kwa nabii Yeremia kusema awaombee kwa Yawe, Mungu wao.


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Hapo, Haruni akamwambia Musa: Ewe bwana wangu, tumetenda mambo ya kipumbafu na kufanya zambi. Lakini usituazibu!


Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye.


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


Halafu Simoni akawaambia Petro na Yoane: “Muniombee ninyi wenyewe kwa Bwana, kusudi lisinipate hata neno moja kati ya maneno haya muliyosema.”


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ