Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:17
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akashuka chini kuona muji ule na munara ambayo wanadamu walijenga.


Basi, Mungu alipomaliza kuongea, akamwacha Abrahamu.


Abramu akaanguka uso mpaka chini. Naye Mungu akamwambia:


Yawe alipomaliza kuzungumuza na Abrahamu, akajiendea naye Abrahamu akarudi kwake.


Wale wanafunzi wa manabii kutoka Yeriko walipomwona, walisema: “Roho wa Elia yuko kwa Elisha.” Basi, wakaenda kumupokea, wakainama mbele yake kwa heshima.


Walipofika ngambo, Elia akamwambia Elisha: “Uniambie jambo unalotaka nikufanyie mbele sijaondolewa kwako.” Elisha akamwambia: “Ninaomba sehemu mara mbili ya roho yako.”


Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria; ukawapa mana kuwa chakula chao, na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.


Utajichokesha mwenyewe na hawa watu, maana hii ni kazi ngumu usiyoweza kuifanya peke yako.


Hao ndio watakaokuwa na vikao kila siku kutatua matatizo ya watu. Matatizo magumu watakuletea wewe, lakini yale madogomadogo watayaamua wenyewe. Kwa njia hiyo utaweza kufanya kazi yako kuwa nyepesi kwa vile watashirikiana nawe katika kazi hiyo.


wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.


Yawe akashuka juu ya mulima Sinai, akamwita Musa kutoka kule juu, naye Musa akapanda juu ya mulima.


Yawe akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Musa, akataja jina lake: Yawe.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Hapo, Yawe akashuka katika wingu na kuzungumuza naye. Halafu akatwaa sehemu ya roho aliyokuwa amemupa Musa, akawapa kila mumoja wa wale wazee makumi saba. Walipoingiwa na roho huyo, wazee hao wakaanza kutoa unabii, lakini hawakurudia kufanya hivyo.


Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele.


Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake,


Wakati Musa alipoingia ndani ya hema la mukutano kwa kuongea na Yawe, akasikia sauti kutoka upande wa juu wa kiti cha rehema, kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano, kutoka kati ya wale makerubi.


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Lakini ninyi sasa hamutawaliwi na hali yenu zaifu ya kimwili, lakini munatawaliwa na Roho Mutakatifu, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Na mutu yeyote asiyekuwa na Roho wa Kristo ndani yake, yeye si mutu wa Kristo.


Na sisi hatukupokea roho ya dunia hii, lakini tulipokea Roho anayetoka kwa Mungu, kusudi tupate kujua vitu vyote tulivyojaliwa kwa neema ya Mungu.


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Watu hawa ndio wanaoleta matengano; wanatawaliwa na tabia za kimwili nao hawana Roho wa Mungu.


Roho wa Yawe atakufikia kwa nguvu, nawe utaanza kutabiri pamoja nao na kugeuka kuwa mutu mwingine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ