Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, Yawe akamwambia Musa: Uwakusanye wazee makumi saba wa Israeli, ambao wewe unajua wanaheshimiwa na kukubaliwa na watu kuwa viongozi, uwalete kwenye hema la mukutano, wasimame karibu nawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:16
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule katika inchi ya Misri Yosefu alikuwa amepata wana wawili. Kwa hiyo watu wote wa jamaa ya Yakobo walioingia Misri walikuwa makumi saba.


Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.


Yawe akamwambia Musa: Mukuje kwangu, wewe Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee makumi saba wa Israeli, muniabudu kwa mbali.


Kisha Musa, Haruni, Nadabu na Abihu na wazee makumi saba wa Israeli wakapanda juu ya mulima,


Kisha Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli.


Yawe akaniambia hivi: Kwenda kununua mutungi kwa mufinyanzi. Kisha, uwatwae wakubwa wamoja wa watu na makuhani waongozi wamoja.


Na mbele yao kulikuwa wazee makumi saba wa taifa la Waisraeli pamoja na Yazania mwana wa Safanu. Kila mumoja alikuwa na chetezo katika mukono, na moshi wa ubani ulipanda juu.


Basi, Musa akaenda na kuwajulisha watu yale Yawe aliyosema. Kisha, akakusanya wazee makumi saba kutoka kati ya wazee viongozi nao akawaweka kandokando kuzunguka hema.


Basi, Musa akaenda kwa Datani na Abiramu, akifuatwa na wazee wa Israeli.


Nyuma ya maneno hayo, Bwana akawachagua watu wengine makumi saba. Naye akawatuma wawili wawili wamutangulie kupita katika kila muji na kila nafasi yeye mwenyewe alipokuwa amekusudia kwenda.


Wale wanafunzi makumi saba wakarudia wakijazwa na furaha, nao wakasema: “Bwana, hata pepo wanatutii tunapowaamuru kwa jina lako!”


Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


Uwakusanye mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na wakubwa wenu nipate kusema maneno haya wasikie, nayo dunia ishuhudie juu yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ