15 Ikiwa hivi ndivyo utakavyonitendea, afazali uniue mara moja! Kama ninapata kukubaliwa mbele yako, usiniache kuendelea katika taabu yangu.
naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”
hata ninaona afazali kutundikwa, ninaona heri kufa kuliko kupata mateso haya.
Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.
Kwa nini mateso yangu hayaishi? Mbona kidonda changu hakiponi nacho hakitaki kutunzwa? Kama vile kijito chenye kukaukakauka, kisivyoweza kutumainiwa, ndivyo wewe umekuwa kwangu!
Kwa nini nilitoka katika tumbo la mama yangu? Nilitoka kusudi nipate taabu na huzuni na kuishi maisha ya haya?
Basi, sasa ee Yawe, ninakusihi uniondoe uzima wangu, maana ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.
Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.
Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.