Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wakaanza kunungunika mbele ya Yawe juu ya taabu zao. Yawe akasikia, na hasira yake ikawaka. Moto toka kwa Yawe ukawaka kati yao na kuchoma upande mumoja wa kambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 11:1
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tendo hilo likamwuzi Yawe, akamwua Onani vilevile.


Muda wa kufunga kilio ulipokwisha, Daudi aliagiza wamulete Batiseba na kumupeleka katika nyumba yake. Batiseba akakuwa muke wa Daudi, naye akamuzalia Daudi mutoto mwanaume. Lakini jambo hilo Daudi alilofanya lilimuchukiza Yawe.


Elia akamujibu: “Kama kweli mimi ni mutu wa Mungu, moto ushuke kutoka mbinguni na kukuteketeza wewe pamoja na watu wako!” Mara moja moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamuteketeza pamoja na watu wake makumi tano.


Alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Umeme wa radi umewachoma na kuwateketeza kondoo na watumishi. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


moto ukawatokea wafuasi wao, ukawateketeza watu hao waovu.


Yawe, aliposikia hayo, akakasirika, moto ukawawakia wazao wa Yakobo, hasira yake ikapanda juu ya watu wa Israeli,


Moto ukawateketeza vijana wao wanaume, na wabinti wao wakakosa wachumba.


Tena, kesho asubui mutaona utukufu wa Yawe maana ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie?”


Kisha Musa akamwambia Haruni: “Uwaambie Waisraeli wote wakusanyike mbele ya Yawe, maana ameyasikia manunguniko yao.”


Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto. Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu, miiba yake na michongoma zake pamoja.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Kwa nini mutu anungunike ikiwa ameazibiwa kwa ajili ya zambi zake?


Kama nilivyowahukumu wazee wenu kule katika jangwa katika inchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Basi, moto ukatokea mbele ya Yawe, ukawateketeza hao vijana, wakakufa mbele yake.


Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Ugonjwa mukali unatangulia mbele yake, nyuma yake hasara inafuata.


Basi, watu wakasafiri toka Sinai, mulima wa Yawe, mwendo wa siku tatu. Sanduku la Agano la Yawe liliwatangulia mwendo wa siku tatu, kwa kuwatafutia pahali pa kupigia kambi.


Sasa uwaambie watu hivi: Mujitakase kwa ajili ya kesho; mutakula nyama. Yawe amesikia mukilia na kusema kwamba hakuna wa kuwapa nyama, na kwamba hali yenu ilikuwa nzuri zaidi mulipokuwa Misri. Sasa Yawe atawapa nyama, nanyi sherti mutaikula.


Wakasema: Basi, Yawe amezungumuza kwa kumwagiza Musa peke yake? Si amezungumuza nasi vilevile? Yawe akasikia maneno hayo.


Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


hakuna hata mumoja wao ambaye amekwisha kuuona utukufu wangu na vitambulisho vyangu nilivyofanya Misri na katika jangwa kisha akazidi kunijaribu mara hizi zote bila ya kutii sauti yangu,


Kundi hili la watu waovu litaendelea kuninungunikia mpaka wakati gani? Nimechoka na haya manunguniko ya Waisraeli juu yangu!


Sasa uwajibu hivi: Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, nitawatendea ninyi yaleyale niliyosikia mukiyasema:


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


Kisha Yawe akashusha moto ukawateketeza wale watu mia mbili makumi tano waliokwenda kufukiza ubani.


Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.


Basi, wakaanza kumunungunikia Mungu na Musa, wakisema: Kwa nini mumetutoa Misri tukuje tukufie humu katika jangwa? Humu hamuna chakula wala maji; nasi tumechokeshwa na chakula hiki cha bure.


Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.


Mukumbuke jinsi walivyowashambulia huko katika njia mukiwa wazaifu na kuwapiga wale wote waliokuja nyuma yenu wamechoka. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


“Tena mulimukasirikisha Yawe, Mungu wenu, huko Tabera, Masa na Kiburoti-Hatawa.


kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ