Yesu akaongeza kusema: “Ninyi munafikiri nini juu ya habari hii? Kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa na watoto wawili. Yeye akamwambia mutoto wa kwanza: ‘Mutoto wangu, ninataka uende leo kutumika katika shamba langu la mizabibu.’
“Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile.
Kwa hiyo basi, tangu sasa hatumuhesabu tena mutu yeyote kufuatana na hali ya kimutu. Hata ikiwa tulimuhesabu Kristo kufuatana na hali ya kimutu, kwa sasa hatumuhesabu tena kufuatana na hali ile.
Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.
Kwa njia ya imani, Abrahamu alitii wakati Mungu alipomwita na kwenda katika inchi ile Mungu aliyoahidi kumupatia kuwa urizi wake. Akaacha inchi yake pasipo kujua pahali anapokwenda.
Wazao wa Keni ambaye alikuwa baba mukwe wa Musa, walifuatana na watu wa kabila la Yuda kutokea Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema muji wa Yeriko, mpaka jangwa la Yuda karibu na Aradi, wakafanya makao yao kule pamoja na watu wa Yuda.