Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Vilevile katika siku zenu za furaha, kama vile sikukuu za mwandamo wa mwezi na sikukuu nyingine, mutapiga baragumu hizi wakati munapotoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani. Hapo mimi Mungu wenu nitawakumbuka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 10:10
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mume wake akamwuliza: “Kwa nini unataka kumwona leo? Leo si sikukuu ya mwandamo wa mwezi wala Sabato.” Akamujibu: “Si neno.”


Sebania, Yosafati, Netaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, waliokuwa makuhani, waliwekwa kwa kupiga baragumu mbele ya Sanduku la Agano. Obedi-Edomu na Yehiya waliwekwa vilevile kuwa walinzi wa sanduku.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika pamoja kwa shangwe kwa kubeba Sanduku la Agano la Yawe mpaka Yerusalema. Wakalisindikiza kwa mulio wa baragumu, ngunga, matoazi, na sauti kubwa za vinanda na vinubi.


Hemani na Yedutuni walikuwa na baragumu na matoazi kwa ajili ya muziki na ala za muziki kwa ajili ya nyimbo takatifu. Wana wa Yedutuni walichaguliwa kwa kulinda milango.


Walawi walisimama na vyombo vya muziki vya Daudi, vilevile makuhani walisimama wakiwa na baragumu zao.


Watu wote waliokuwa mule wakashiriki katika ibada. Waimbaji wakaendelea na kuimba, na baragumu zikaendelea kupigwa mpaka wakati shuguli za utoaji wa sadaka hiyo ya kuteketeza kwa moto ilipokamilika.


Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.


Wajengaji walipoanza kuweka musingi wa hekalu la Yawe, makuhani wakiwa wamevaa nguo zao, walisimama pahali pao na baragumu katika mikono, nao Walawi wa ukoo wa Asafu wakisimama na matoazi yao, basi, wakamutukuza Yawe kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi wa Israeli.


Wazao hawa wa makuhani walikuwa na baragumu: Zakaria, mwana wa Yonatani mujukuu wa Semaya aliyekuwa mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu.


Mumusifu kwa mulio wa baragumu, mumusifu kwa zeze na kinubi!


muvumishe wimbo wa shangwe, mupige ngoma, mucheze zeze na kinubi cha sauti nzuri.


Mupige baragumu kutangaza mwandamo wa mwezi, na pia mbalamwezi wakati wa sikukuu yetu.


Haki na sheria ndio musingi wa utawala wako; wema na uaminifu vinakutangulia!


Haruni anapoingia Pahali Patakatifu, atavaa kifuko cha shauri ambacho juu yake kulichorwa majina ya makabila ya wana wa Israeli. Kwa namna hiyo mimi Yawe sitawasahau ninyi hata kidogo.


Wewe utaipokea feza hiyo ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli, nawe utaitumia kwa shuguli za kazi za hema takatifu, nayo ikuwe ni ukumbusho wa Waisraeli mbele yangu, malipo ya maisha yenu.


Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa saba mutafanya siku ya mapumziko, siku ya ukumbusho itakayotangazwa kwa mulio wa baragumu na kufanya mukutano mutakatifu.


Wakati wa vita katika inchi yenu juu ya waadui wanaowashambulia, mutatoa kitambulisho cha vita kwa kupiga baragumu hizi kusudi Yawe, Mungu wenu apate kuwakumbuka na kuwaokoa na waadui zenu.


Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.


Siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi. Hiyo ni siku ya kupiga baragumu.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.


kwa rafla, kama vile mutu anavyofunga jicho na kulifungua, wakati ngunga ya mwisho itakapolia. Kwa maana wakati itakapolia, wafu watafufuka na kupata kuwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi wote tutabadilishwa.


Kwa sababu amri itakapotoka na sauti ya malaika mukubwa itakaposikilika, na baragumu ya Mungu itakapolia, Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni. Halafu wale waliokufa wakimwamini Kristo watafufuliwa kwanza.


Ninyi mutawaambia: ‘Sanduku la Agano la Yawe lilipopitishwa katika muto Yordani, maji ya muto huo yalizuiliwa yasitiririke!’ Kwa hiyo mawe haya yatakuwa ukumbusho kwa Waisraeli milele.”


Makuhani saba, kila mumoja akiwa anabeba baragumu yake ya pembe ya kondoo dume, watatangulia mbele ya Sanduku la Agano. Katika siku ya saba mutauzunguka muji ule mara saba, nao makuhani wakipiga mabaragumu.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Daudi akamwambia: “Kesho ni sikukuu ya mwandamo wa mwezi, nami nilipaswa kuwa kwenye meza kwa kula pamoja na mufalme. Lakini uniache, niende kujificha kule katika shamba mpaka siku ya tatu magaribi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ