Hesabu 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Yawe akamwambia Musa: အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye kiingilio cha hekalu kama ilivyokuwa desturi nao wakubwa wa waaskari na wapiga baragumu wakiwa pembeni ya mufalme, na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu. Basi, akapasua nguo zake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”
Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye mulango, wakati majemadari na wapiga baragumu wakiwa kando ya mufalme na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu; nao waimbaji wakiwa na ala zao za muziki wakiongoza watu katika sherehe; halafu akapasua nguo yake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”
Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.