Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 1:53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

53 Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 1:53
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, ilikuwa ni kazi yao kutunza hema la kusanyiko na Pahali Patakatifu, na kuwasaidia wandugu zao makuhani, wazao wa Haruni, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe.


“Lakini kwa ngambo yetu, Yawe ni Mungu wetu, wala hatujamwacha. Tena tuko na makuhani wa uzao wa Haruni ambao wanamutumikia Yawe, nao wanasaidiwa na Walawi.


Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya manabii wa Yerusalema: Nitawakulisha uchungu, na kuwapa maji yenye sumu wakunywe. Maana kutoka kwa manabii wa Yerusalema kutomwogopa Mungu kumeenea kila pahali katika inchi.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.


Utawachagua wakuwe waangalizi wa hema la kuchunga vibao vya agano, vyombo vyake vyote na kila kitu kinachokuwa ndani yake; watakuwa wakilibeba pamoja na vyombo vyake vyote. Watatumika mule ndani na watapiga kambi yao kwa kulizunguka.


Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Munaona ni jambo dogo kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewachagua ninyi kati ya Waisraeli wote, kusudi muweze kumukaribia na kutumika katika hema la Yawe na kushugulika na kutumikia Waisraeli wote?


Walipokusanyika mbele ya Musa na Haruni kwa kutoa malalamiko yao, wakageuka kuelekea hema la mukutano, wakaona kwamba wingu limeifunika hema na utukufu wa Yawe ulikuwa umetokea pale.


Halafu, kambi ya kabila la Walawi likiwa katikati ya kambi zote nao wakibeba hilo hema la mukutano wataondoka; kila kundi likisafiri kwa kufuata nafasi yake kwa bendera.


Ilipasa kwa jamaa za Wagersoni kupiga kambi yao upande wa magaribi, nyuma ya hema takatifu


Jamaa za wana wa Kohati watapiga kambi yao upande wa kusini wa hema takatifu,


Mukubwa wa ukoo wa jamaa za Merari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa watapiga kambi yao upande wa kaskazini wa hema takatifu.


Musa na Haruni na wana wao watapiga kambi yao mbele ya hema takatifu upande wa mashariki, ni kusema mbele ya hema la mukutano kuelekea upande linakotokea jua. Kazi yao itakuwa kutumika kwenye Pahali Patakatifu kwa jambo lolote lililohitajika kufanyika kwa ajili ya Waisraeli. Mutu mwingine yeyote aliyesogea karibu alipaswa kuuawa.


Kutoka katika lile fungu la jamii nzima, utwae mumoja kati ya kila makumi tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo na mbuzi. Hivyo utawapa Walawi ambao wanashugulika na kazi katika hema la Yawe.


Kutoka nusu hii Waisraeli waliyopewa, Musa alitwaa mumoja kati ya kila mateka makumi tano na nyama makumi tano, kama alivyoamriwa na Yawe, akawapa Walawi ambao walitumika katika hema la Yawe.


na nimewatoa kwa Haruni na wana wake, kama vile zawadi kutoka kwa Waisraeli, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano kwa ajili ya Waisraeli na kuwafanyia upatanisho kusudi kusitokee pigo kati ya Waisraeli wakikaribia Pahali Patakatifu.


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ