Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 1:50 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

50 Utawachagua wakuwe waangalizi wa hema la kuchunga vibao vya agano, vyombo vyake vyote na kila kitu kinachokuwa ndani yake; watakuwa wakilibeba pamoja na vyombo vyake vyote. Watatumika mule ndani na watapiga kambi yao kwa kulizunguka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 1:50
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi mufalme akamwita kiongozi Yoyada, akamwuliza: “Mbona haujaamurisha Walawi kukusanya kutoka kwa watu wa Yuda na Yerusalema, kodi ambayo Musa mutumishi wa Yawe aliagiza watu walipe kwa ajili ya Hema Takatifu la Yawe?”


Wakati wa Eliasibu, Yoyada, Yohanani na Yadua wakubwa wa jamaa za Walawi waliandikwa; vilevile wakati wa utawala wa mufalme Dario wakubwa wa jamaa za makuhani waliandikwa.


Watu wote wa Israeli, tangu wakati wa Zerubabeli na Nehemia, walitoa matoleo ya kila siku kwa ajili ya waimbaji na walinzi wa milango. Zaidi ya yote, watu wa Israeli wakatoa matoleo kwa ajili ya Walawi, nao Walawi wakatenga sehemu kwa ajili ya wazao wa Haruni.


Walawi walikuwa: Yesua, Binui, Kadimieli, Serebia, Yuda na Matania, ambaye alishugulika na usimamizi wa nyimbo za shukrani akishirikiana na ndugu zake.


Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.


alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.


Humo ndimo makabila yanamofika, ndiyo, makabila ya Yawe, kwa kumushukuru Yawe kama Waisraeli walivyoagiza.


Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.


Hii ndiyo hesabu ya vifaa vilivyotumika katika kujenga hema la kuchunga vile vibao vya agano. Hesabu hii ilitayarishwa na Walawi kwa amri ya Musa, chini ya uongozi wa Itamari mwana wa kuhani Haruni.


Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli.


Kisha walifuata watu wa ukoo wa Kohati, wakiwa wamebeba vyombo vitakatifu. Walipofika, hema lilikuwa limekwisha kusimikwa.


Walipokusanyika mbele ya Musa na Haruni kwa kutoa malalamiko yao, wakageuka kuelekea hema la mukutano, wakaona kwamba wingu limeifunika hema na utukufu wa Yawe ulikuwa umetokea pale.


Ninyi mutafanya kazi za Pahali Patakatifu na mazabahu, kusudi kasirani yangu isiwatokee tena Waisraeli.


Halafu, kambi ya kabila la Walawi likiwa katikati ya kambi zote nao wakibeba hilo hema la mukutano wataondoka; kila kundi likisafiri kwa kufuata nafasi yake kwa bendera.


Kisha Musa akainua mukono wake, akapiga lile jiwe mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika kwa wingi, watu wakakunywa pamoja na mifugo yao.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


utahesabu wanaume wote wenye umri kati ya miaka makumi tatu na makumi tano wanaofaa kujiunga na kazi ya hema la mukutano.


na nimewatoa kwa Haruni na wana wake, kama vile zawadi kutoka kwa Waisraeli, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano kwa ajili ya Waisraeli na kuwafanyia upatanisho kusudi kusitokee pigo kati ya Waisraeli wakikaribia Pahali Patakatifu.


Kwa hiyo Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja wakatakasa Walawi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Kisha hayo Walawi wakaingia na kufanya kazi yao katika hema la mukutano chini ya usimamizi wa Haruni na wana wake, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Na nyuma ya pale nikaona hekalu limefunguliwa mbinguni; mule mulikuwa hema yenye vibao vya agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ