Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wale wote katika Israeli wanaoweza kwenda kwa vita, wenye umri kuanzia miaka makumi mbili na zaidi, mutawaweka katika hesabu ya majeshi yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 1:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yoabu alimupelekea mufalme jumla ya watu. Katika inchi ya Israeli kulikuwa wanaume mashujaa elfu mia ine wenye ujuzi wa kutumia mapanga; na katika Yuda, kulikuwa wanaume elfu mia tano.


Makabila ya Rubeni, Gadi na Manase ya upande wa mashariki, yalikuwa na waaskari shujaa yapata elfu makumi ine na ine mia saba na makumi sita, wenye ngao na mapanga, wavuta pinde wafundi katika vita.


Mufalme Amazia akawakusanya wanaume wa Yuda, akawapanga katika vikundi mbalimbali kulingana na ukoo zao, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na wa mamia kwa ajili ya Yuda na Benjamina. Alipowakagua wale wenye miaka makumi mbili na zaidi, akapata watu elfu mia tatu kwa jumla. Wote walikuwa watu waliochaguliwa wanaofaa kwa vita, wanaoweza kutumia mikuki na ngao.


Mutashika sikukuu hii ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama ukumbusho wa siku nilipowatoa ninyi vikundi vya Israeli kutoka Misri. Sikukuu hiyo itashikwa na vizazi vyenu vyote vinavyokuja, kama agizo la milele.


Kila mumoja atakayehesabiwa, tangu umri wa miaka makumi mbili na zaidi, atanitolea sadaka hiyo.


Kila mutu aliyehesabiwa tangu umri wa miaka makumi mbili na moja na zaidi alitoa muchango wake wa feza grama tano. Wanaume wote waliohesabiwa walikuwa elfu mia sita na tatu na mia tano na makuni tano.


Mutakufa na miili yenu itatupwa humuhumu katika jangwa, kwa sababu mumenungunika juu yangu, hakuna hata mumoja wenu mwenye umri wa kuanzia miaka makumi mbili na zaidi,


Muhesabu Waisraeli wote, kila mutu kufuatana na jamaa yake. Muwahesabu watu wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi wanaofaa kwenda katika jeshi.


Uwahesabu wana wa Walawi wote kulingana na ukoo zao na jamaa zao, kila mwanaume kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi.


Hakika hakuna mutu yeyote kati ya watu waliotoka Misri mwenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi atakayeona inchi niliyoapa kuwapa Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwa sababu hawakunitii kwa ukamilifu.


Hivi ndivyo vituo ambavyo Waisraeli wakapiga kambi walipotoka Misri wakiwa katika makundi ya makabila yao chini ya uongozi wa Musa na Haruni.


utahesabu wanaume wote wenye umri kati ya miaka makumi tatu na makumi tano wanaofaa kujiunga na kazi ya hema la mukutano.


“Mwanaume aliyetoka kuoa asiende kwa vita wala asipewe kazi yoyote ingine; aachwe huru kwa muda wa mwaka mumoja, kusudi akae kwake na kufurahi na muke wake.


“Wakati ule niliwapa maagizo haya: ‘Yawe, Mungu wenu amewapa inchi hii upande wa mashariki wa muto Yordani ikuwe mali yenu. Sasa ninyi mashujaa kati ya wandugu zenu, mutwae silaha muvuke muto Yordani mukiwa mbele ya wandugu zenu Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ