Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hesabu 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hesabu 1:1
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Solomono alianza kujenga nyumba ya Yawe katika mwaka wa mia ine na makumi nane kisha Waisraeli kutoka Misri. Huo ulikuwa mwaka wa ine wa utawala wa Solomono juu ya Israeli, katika mwezi wa Zivu, ni kusema mwezi wa pili.


Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu tangu walipotoka katika inchi ya Misri, watu wa Israeli wakafika katika jangwa la Sinai.


Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, kule wakapiga kambi mbele ya mulima Sinai.


Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza mwaka wa pili kisha kutoka Misri, hema takatifu likasimikwa.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimika hema takatifu la mukutano.


Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:


Hizo ndizo amri ambazo Yawe alimwamuru Musa kusudi awaambie Waisraeli kwenye mulima Sinai.


Na katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, wakakusanya Waisraeli wote. Waliandika majina ya wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi, kulingana na jamaa zao na ukoo zao,


Halafu kwa rafla, Yawe akawaambia Musa, Haruni na Miriamu: Mukuje katika hema la mukutano, ninyi watatu. Basi, wote watatu wakaenda kwenye hema la mukutano.


Kisha katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili nyuma ya Waisraeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa katika jangwa la Sinai. Akamwambia:


Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, mwaka wa makumi ine nyuma ya kutoka Misri, Musa akawaambia watu kila kitu ambacho Yawe alimwamuru awaambie.


Miaka makumi tatu na nane ilikuwa imepita tangu kuondoka Kadesi-Barnea mpaka kuvuka kijito Zeredi. Wakati huo, wote wenye umri wa kwenda kwa vita waliotoka Misri walikuwa wamekwisha kufa, kulingana na jinsi Yawe alivyowaapia.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ