Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hagai 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Hagai akajibu na kusema hivi: Hivi ndivyo inavyokuwa kwa watu wa taifa hili mbele yangu –ni ujumbe wa Yawe– na kila kitu wanachofanya; hata vitu wanavyotoa kwenye mazabahu ni vichafu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hagai 2:14
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.


Anayekataa kuisikia sheria, yule, hata maombi yake, ni chukizo kwa Mungu.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai, wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao. Chakula chao kitakuwa kama cha kilio, wote watakaokikula watajichafua. Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu, hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


muwaokoe, mukiwaopoa toka katika moto. Muwasikilie vilevile wengine huruma, lakini kwa woga, mukichukia hata nguo zao zilizochafuliwa na tamaa zao mbaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ