Basi, akaniambia hivi: Wewe mwanadamu! Angalia vizuri na kusikiliza kwa uangalifu. Shika kwa moyo uone kila kitu nitakachokuonyesha maana umeletwa hapa kusudi nikuonyeshe kitu. Unapaswa kuwatangazia watu wa Israeli kila kitu utakachoona.
Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.
Wakamwambia mufalme: Yule Danieli anayekuwa mumoja wa wafungwa kutoka inchi ya Yuda hakuheshimu wewe mufalme wala amri uliyotia sahihi. Anafanya maombi yake mara tatu kila siku.
Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.
Mujichunguze ninyi wenyewe kusudi mupate kujua kama munasimama imara katika imani. Mujipime. Si munajua kwamba Yesu Kristo anakaa kati yenu? Kama si vile ni kusema kwamba mumeshindwa.
Kila mutu achunguze mwenendo wake mwenyewe. Basi akiwa na sababu ya kujivuna, ajivune kufuatana na mwenendo wake mwenyewe pasipo kujilinganisha na mutu mwingine.