Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hagai 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ni sawa kwenu kukaa katika nyumba zenu nzuri wakati nyumba yangu ni mabomoko matupu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hagai 1:4
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mufalme Daudi akamwambia nabii Natani: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba iliyojengwa na miti ya mierezi, lakini Sanduku la Mungu linakaa ndani ya hema.”


Lakini Elisha akamwambia: “Unafikiri roho yangu haikukuwa pamoja nawe wakati mutu yule alipotoka ndani ya gari lake na kuja kukutana nawe? Huu ndio wakati wa kupokea feza na nguo, mashamba ya mizeituni na mizabibu, kondoo na ngombe au watumishi na wajakazi?


Wewe utasimama na kurehemu Sayuni, maana wakati umefika wa kuuhurumia, wakati wake uliopangwa umefika.


Waliunguza pahali patakatifu pako; walikufuru pahali pale unapoheshimiwa.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Wewe unayesema: Nitajijengea nyumba kubwa, yenye vyumba vikubwa vya magorofi. Kisha unaifanyia madirisha, ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi, na kuipaka rangi nyekundu!


Katika siku Hezekia alipokuwa mufalme wa Yuda, Mika wa Moreseti aliwatangazia watu wote kwamba Yawe wa majeshi alisema hivi: Sayuni utalimiwa kama shamba, Yerusalema utabaki mabomoko, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


basi, nitaiharibu nyumba hii kama nilivyoharibu ile ya Shilo, na nitaufanya muji huu kuwa mufano kwa mataifa yote ya dunia yatakaoutumia kwa kutoa laana.


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


Yawe wa majeshi anasema hivi: Pahali hapa ambapo ni jangwa bila watu wala nyama, na katika miji yake yote, patakuwa shamba ambalo wachungaji watakulisha ndani yake makundi yao ya kondoo.


Aliteketeza kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa ilichomwa kwa moto.


Yawe amechukia mazabahu yake na hekalu lake amelikataa. Amewaachilia waadui wazibomoe kuta za nyumba zake katika muji. Wakapiga kelele ndani ya nyumba ya Yawe kama kelele za wakati wa sikukuu.


Namna gani zahabu yetu ilivyochakaa, zahabu safi kabisa ilivyobadilika! Mawe ya bei kali yamesambazwa kwa barabara zote.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai kusema hivi:


Basi, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri vizuri juu ya namna munavyofanya!


Mulitazamia mavuno mengi, lakini mulipata kidogo tu. Mulipoyaleta kwenye nyumba, niliyapeperusha mbali. Kwa nini? Kwa sababu nyumba yangu ni mabomoko matupu wakati kila mumoja wenu anashugulikia nyumba yake.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Watu wengine wote wanatafuta faida yao wenyewe, lakini hawashuguliki na Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ