Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hagai 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu hawa wanasema kwamba wakati wa kuijenga upya nyumba ya Yawe haujafika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hagai 1:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hata nyuma ya miaka makumi mbili na mitatu ya utawala wa Yoasi, makuhani walikuwa bado hawajatengeneza hata mabomoko ya nyumba.


Mara tu waliposomewa barua hii kutoka kwa Artasasta, Rehumu, karani Simusayi na wenzao wakaharakisha kwenda Yerusalema na kuwalazimisha kwa nguvu Wayuda waache kuujenga muji.


Tokea siku ile na kuendelea, nusu ya watumishi wangu wakakuwa wanaendelea na ujenzi wakati nusu ingine ikakuwa inashika ulinzi wakiwa na mikuki, ngao, pinde na nguo za chuma. Viongozi wetu wakakuwa upande wa watu wa Yuda


Muvivu anasema: “Kuna simba inje. Nitauawa katika njia.”


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Anayechunguza upepo hatapanda mbegu, anayeangalia mawingu yatoweke, hatavuna kitu.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai kusema hivi:


Lakini watu walioandamana naye kupeleleza inchi wakasema: Hatutaweza kupigana na watu hao; wao wana nguvu kuliko sisi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ