Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Tangu nyakati za babu zetu mpaka sasa, sisi watu wako tumekukosea sana. Na kwa sababu ya zambi zetu, sisi, wafalme wetu na makuhani wetu tulitiwa katika mikono ya wafalme wa inchi za kigeni, tukauawa, tukapelekwa kuwa wafungwa na kunyanganywa mali zetu. Na hata hivi leo, tumetiwa haya kupita kiasi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 9:7
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Kwa maana babu zetu waliasi na kutenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wetu. Wamemwacha na kugeuzia mbali nyuso zao na makao ya Yawe.


Musikuwe kama babu zenu na wandugu zenu ambao hawakukuwa waaminifu kwa Yawe Mungu wa babu zao, ambaye kama vile munavyoona aliwaazibu vikali.


Yawe anasema hivi: ‘Angalia nitaleta uovu juu ya Yerusalema na juu ya wakaaji wake, laana zote zilizoandikwa katika kitabu kilichosomwa mbele ya mufalme wa Yuda.


Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Ukawavumilia kwa miaka mingi, na kuwaonya kwa njia ya roho wako kwa kupitia manabii wako; hata hivyo hawakusikiliza. Basi ukawaacha ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Kwanza nikakunywesha wakaaji wa Yerusalema na miji mingine ya Yuda, wafalme wake na wakubwa wa serikali yake kusudi ikuwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na cha kulaaniwa, kama inavyokuwa mpaka leo. Halafu nikakunywesha:


Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.


Mumesahau uovu wa babu zenu, uovu wa wafalme wa Yuda, uovu wa wake wao na uovu wenu ninyi wenyewe na wa wake wenu, ambao muliufanya katika inchi ya Yuda na kwenye barabara za Yerusalema?


Babu zetu walitenda zambi na sasa hawako tena; nasi tunabeba makosa yao.


Nitawatoa ndani ya muji na kuwatoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine, nami nitawahukumu.


Mataifa yatajua kwamba Waisraeli walikwenda katika uhamisho kutokana na makosa yao wenyewe waliyonikosea. Waliniasi, nami nikageuka wasipate kuniona, nikawatoa katika mikono ya waadui zao wakauawa.


Na sasa, enyi kizazi cha wenye zambi, mumesimama kwa pahali pa wazee wenu, kuongeza tena hasira kali ya Yawe juu ya Waisraeli.


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ