Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 9:6
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Lakini kule Samaria kulikuwa nabii wa Yawe, jina lake Obedi. Yeye alitoka kwenda kukutana na waaskari wa Israeli walipokuwa karibu kuingia Samaria, akawaambia: “Yawe, Mungu wa babu zenu, alikuwa amewakasirikia watu wa Yuda, ndiyo maana aliwatia katika mikono yako lakini umewaua kwa hasira. Tendo hilo limetoka mbinguni.


Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.


Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini? Ninafunga kinywa changu.


Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu; ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.


Hakuna uzima katika mwili wangu, kwa sababu umenikasirikia. Hakuna afya hata katika mifupa yangu, kwa sababu ya zambi yangu.


Nimefunikwa kabisa na zambi zangu, zinanilemea kama muzigo muzito sana.


Hivyo Musa akarudi kwa Yawe, akamwambia: Ninasikitika! Watu hawa wametenda zambi kubwa. Wamejifanyia wenyewe miungu ya zahabu.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Makosa yetu mbele yako ni mengi sana, zambi zetu zinashuhudia juu yetu. Kweli, makosa yetu yanaandamana nasi, tunayajua maovu yetu.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Maana kisha kukuasi, niligeuka toka zambi zangu, na kisha kufundishwa, nilijilaumu, nikapata haya na kufezeheka, maana nilibeba haya za ujana wangu.


Tulijaribu kuuponyesha Babeli, lakini hauwezi kupona. Muuache, tujiendee, kila mumoja katika inchi yake. Hukumu yake ni kubwa sana inafika mpaka katika mawingu.


Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo? Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka; wakati nitakapowaazibu, wataangamizwa kabisa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Tulikukosea na kukuasi, nawe haujatusamehe bado.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Lakini kama wakitubu uovu wao na uovu wa wazee wao juu ya uasi waliotenda juu yangu na vilevile juu ya kupingana kwao nami,


Mwana wake akamwambia: ‘Baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile. Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako.’


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!


Kwa maana zambi zake zinazidi sana hata zimefika mbinguni na Mungu hakusahau mabaya yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ